Bonyeza Hapa - Alhidaaya.com
Transkript
Bonyeza Hapa - Alhidaaya.com
VIPI UWEZE KUHIFADHI QUR-AAN? Ummu Iyyaad: 1 www.alhidaaya.com 01- Yaliyomo 02- Utangulizi 03- Fadhila Za Kusoma Na Kuhifadhi Qur-aan 04- Umri Bora Wa Kuhifadhi Qur-aan 05- Nasaha Za Kuhifadhi Qur-aan 06- Utaratibu Wa Kuhifadhia Qur-aan 07- Zingatia Aayah Zinazofanana 08- Kuithibitisha Qur-aan Baada Ya Kuihifadhi 09- Hitimisho: 2 www.alhidaaya.com 02-Utangulizi: Qur-aan, maneno ya Allaah ()سبحانه وتعالى, Aliyopelekewa Wahyi Mtume ( )صلى ﷲ عليه وآله وسلمkupitia Jibriyl ‘alayhis-salaam, akawasomea Maswahaba, nao wakawasomea waliofuatia, ikaendelea kusomwa na kufundishwa hadi kutufikia sisi. Ni Hidaaya kwetu, ni Nuru inanawirisha nyoyo zetu, ni kamba nene inayounganisha Waislamu, ni miyzani ya uadilifu, ni poza ya moyo ya kila aina ya maradhi; kufru, shirki, unafiki, uhasidi, uchoyo na inatibu kila aina ya maasi na maovu. Imejaa hikma katika Aayah zake, Shari’ah zake ambazo zinamfaa bin-Aadam wakati wowote, zama zote, na popote alipo. Amri na makatazo Yake Allaah ( سبحانه )وتعالىhumo pamoja na kumtii Mtume ( )صلى ﷲ عليه وآله وسلمni sababu ya furaha na kufaulu kwa binaadamu katika dunia yake na Akhera yake. Anasema Allaah ()سبحانه وتعالى: ×πuΗ÷qu‘uρ “Y‰èδuρ Í‘ρ߉Á9$# ’Îû $yϑÏj9 Õ!$xÏ©uρ öΝà6În/§‘ ÏiΒ ×πsàÏãöθ¨Β Νä3ø?u!$y_ ô‰s% â¨$¨Ζ9$# $pκš‰r'¯≈tƒ 〈 ∩∈∇∪ tβθãèyϑøgs† $£ϑÏiΒ ×ö&yz uθèδ (#θãmtøu‹ù=sù y7Ï9≡x‹Î7sù ϵÏFuΗ÷qtÎ/ρu «!$# È≅ôÒxÎ/ ö≅è% ∩∈∠∪ tÏΨÏΒ÷σßϑù=Ïj9 Enyi watu! Kwa yakini yamekujieni Mawaidha (Qur-aan inayoamrisha mema na kukataza maovu) kutoka kwa Mola wenu, na Shifaa (poza) ya yale (maradhi) yote yaliyomo vifuani, na Hidaayah na Rahmah kwa Waumini. Sema: (ee Muhammad ): “Kwa fadhila za Allaah na kwa Rahmah Yake (Qur-aan, Uislamu, Iymaan), basi kwa hayo wafurahi.” Hayo ni kheri kuliko wanayoyakusanya (mali na starehe za dunia)1. Lakini manufaa na fadhila hizo haziwezi kumfikia mtu isipokuwa kwa atakayeisoma Qur-aan kwa njia itakayomridhisha Allaah ( سبحانه )وتعالى, Naye Anasema: 1 Yuwnus (10: 57-58) 3 www.alhidaaya.com 〈 3 ϵÎ/ tβθãΖÏΒ÷σムy7Íׯ≈s9'ρé& ÿϵÏ?uρŸξÏ? ¨,ym …çµtΡθè=÷Gtƒ |=≈tGÅ3ø9$# ãΝßγ≈oΨ÷-s?#u tÏ%©!$# Wale Tuliowapa Kitabu wanakisoma kwa haki ya kukisoma kwake (ipasavyo); hao ndio wanaokiamini2 Kitabu hiki In Shaa Allaah, kitaweza kumsaidia anayetaka kuhifadhi Qur-aan pindi mtu akiweka azimio la nguvu na kuanza kwanza Niyya safi moyoni, kuomba du’aa, kufanya juhudi kubwa, kuendelea nayo hifdhi yake bila ya kukata tamaa na kuithibitisha baada ya kuihifadhi. Hapo ndipo itakapomthibitikia kauli ya Allaah ( ) iliyokariri mara nne katika Suwratul-Qamar: 〈 ∩⊇∠∪ 9Ï.£‰•Β ÏΒ ö≅yγsù Ìø.Ïe%#Ï9 tβ#uöà)ø9$# $tΡ÷œ£o„ ô‰s)s9uρ (Na kwa yakini Tumeifanya Qur-aan sahali kuikumbuka [kuisoma, kuihifadhi na kuifahamu], basi je, yuko yeyote anayekumbuka [na kuwaidhika?))]3 Namuomba Allaah ( ) Ajaalie kazi hii iwe kwa ajili ya kupata Radhi Zake Pekee na Ajaalie iwe yenye manufaa kwa ndugu zetu wa Kiislamu na namuomba Atughufurie na Atusamehe kwa makosa yoyote yatakayokuwemo. Wa-Swalla-Allaahu ‘alaa Muhammad wa ‘alaa aalihi wa Swahbihi wa sallam. Ummu Iyyaad–Talha Muhammad Al-Haamid Abu Bakr bin Saalim 20 Rabiy’ul Awwal 1434– 2 Februari 2003 2 3 Al-Baqarah (2: 121) Al-Qamar: (54: 17, 22, 32, 40) 4 www.alhidaaya.com 03- Fadhila Za Kusoma Na Kuhifadhi Qur-aan Allaah Amewafanyia wema mkubwa na ihsaan Waumini kwa kuwaletea Maneno Yake Mwenyewe kwa namna ya kuweza kusomeka na kusikilizika Aayah Zake, na kufikia kumpelekea msomaji au msikilizaji kuhisi kuwa anasemeshwa na Muumba wake na kumsikiliza. Hili ndilo linaloipa na kuitunuku Qur-aan nafasi isiyokadirika kwa Muumini kwani wote wanaamini kuwa Qur-aan ni Maneno ya Allaah yaliyoteremshwa kwa Mtume ( ) kupitia kwa Jibril ( !" ) na kusomwa kwake ni ‘ibaadah. Moja kati ya amri tatu alizoamrishwa Mtume ( ) na Allaah kama inavyobainisha Qur-aan katika Aayah ya SuwratunNaml ni kuisoma Qur-aan. Anasema Allaah (#$ %#&): y Ρ¯ )Î zΒÏ β t θ.ä &r β ÷ &r N ß ö ΒÏ &é ρu ( & ó « x ≅ ‘ 2 à …&ã !s ρu $γ y Βt § m y “% Ï !© #$ οÍ $ t #ù 7t 9ø #$ νÍ ‹ É ≈δ y U & ‘u ‰ y 6ç ã ô &r β ÷ &r N ß ö ΒÏ &é $! ϑ (β t #u ö ) à 9ø #$ #( θu =è ?ø &r β ÷ &r ρu ∩⊇∪ t ϑ Ï =Î ¡ ó ϑ ß 9ø #$ (([Sema ee Muhammad ] “Hakika nimeamrishwa nimwabudu Mola wa huu mji [Makkah] Ambaye Ameufanya mtakatifu [kwa Amri Yake]. Naye ni Vyake Pekee kila kitu. Na nimeamrishwa kwamba niwe miongoni mwa Waislamu” [wanaojisalimisha]. Na kwamba nisome Qur-aan”))4 Akaamrishwa tena kwamba: ( οn θ4 =n Á ¢ 9#$ Ο É %Ï &r ρu = É ≈Gt 3 Å 9ø #$ ∅ š ΒÏ 7 y ‹ø 9s )Î z r Ç ρ&é $! Βt ≅ ã ?ø #$ ((Soma [ee Muhammad ] uliyofunuliwa Wahyi kwako katika Kitabu [Qur-aan] na simamisha Swalaah))5 Japokuwa Qur-aan iliteremshwa kwake ( ), bila shaka Waumini wanaingia katika hilo. 4An-Naml: (27: 91-92) (29: 45) 5Al-‘Ankabuut 5 www.alhidaaya.com Katika majukumu mengine aliyopewa Mtume ( ) kwa Waumini yenye kufungamana na Qur-aan baada ya kutakiwa kuisoma yeye mwenyewe ( ), ni kuwasomea na kuwafunza kuweza kuisoma Qur-aan kama alivyosomewa. Allaah (#$ %#&) Ametaja hilo katika Aayah tatu zilizofanana takriban kwa ukaribu sana, na ya nne ni du’aa ambayo baba wa Mitume Nabii Ibraahiym ( !" ) alikuwa akiiomba na Allaah ( ) kwa Rahmah na Fadhila Zake Akaitakabali na matokeo yake ni kuletwa kwetu Mtume Muhammad ( ): Anasema Allaah ( %#& #$): y7¨ΡÎ) 4 öΝÍκ@Ïj.t“ãƒuρ sπyϑõ3Ïtø:$#uρ |=≈tGÅ3ø9$# ÞΟßγßϑÏk=yèãƒuρ y7ÏG≈tƒ#u öΝÍκö@n=tæ (#θè=÷Gtƒ öΝåκ÷]ÏiΒ Zωθß™u‘ öΝÎγ‹Ïù ô]yèö/$#uρ $uΖ−/‘u ∩⊇⊄∪ ÞΟŠÅ3ysø9$# Ⓝ͕yèø9$# |MΡr& ((Mola wetu, Peleka kwao Mtume miongoni mwao ataewasomea Aayah Zako na ataewafunza Kitabu na Hikmah na atakayewatakasa. Hakika Wewe ni Al-’Aziyzul-Hakiym [Mwenye Nguvu, Mshindi Asiyeshindika daima - Mwenye Hikma wa yote daima])).” 6 |=≈tGÅ3ø9$# ãΝà6ßϑÏk=yèãƒuρ öΝà6ŠÏj.t“ãƒuρ $oΨÏG≈tƒ#u öΝä3ø‹n=tæ (#θè=÷Gtƒ öΝà6ΖÏiΒ Zωθß™u‘ öΝà6‹Ïù $uΖù=y™ö‘r& !$yϑx. ∩⊇∈⊇∪ tβθßϑn=÷ès? (#θçΡθä3s? öΝs9 $¨Β Νä3ßϑÏk=yèãƒuρ sπyϑò6Ïtø:$#uρ ((Kama Tulivyomtuma kwenu Mtume anayetokana na nyinyi, anawasomea Aayah Zetu na anakutakaseni na anakufunzeni Kitabu na Hikmah, na anakufundisheni mambo ambayo hamkuwa mkiyajua))7 6Al-Baqarah: 7 (2: 129) Al-Baqarah (2: 151) 6 www.alhidaaya.com öΝÍκ@Åe2t“ãƒuρ ϵÏG≈tƒ#u öΝÍκö@n=tæ (#θè=÷Gtƒ ôΜÎγÅ¡àΡr& ôÏiΒ Zωθß™u‘ öΝÍκ@Ïù y]yèt/ øŒÎ) tÏΖÏΒ÷σßϑø9$# ’n?tã ª!$# £tΒ ô‰s)s9 ∩⊇∉⊆∪ AÎ7•Β 9≅≈n=|Ê ’Å∀s9 ã≅ö6s% ÏΒ (#θçΡ%x. βÎ)uρ sπyϑò6Ïtø:$#uρ |=≈tGÅ3ø9$# ãΝßγßϑÏk=yèãƒuρ ((Kwa yakini Allaah Amewafadhilisha Waumini pale Alipomtuma miongoni mwao Mtume kutokana na nafsi zao; anawasomea Aayah Zake na anawatakasa na anawafunza Kitabu na Hikmah; japokuwa walikuwa kabla katika upotofu bayana))8 sπyϑõ3Ïtø:$#uρ |=≈tGÅ3ø9$# ãΝßγßϑÏk=yèãƒuρ öΝÍκ@Ïj.t“ãƒuρ ϵÏG≈tƒ#u öΝÍκö@n=tã (#θè=÷Ftƒ öΝåκ÷]ÏiΒ Zωθß™u‘ z↵Íh‹ÏiΒW{$# ’Îû y]yèt/ “Ï%©!$# uθèδ ∩⊄∪ &Î7•Β 9≅≈n=|Ê ’Å∀s9 ã≅ö6s% ÏΒ (#θçΡ%x. βÎ)uρ ((Yeye Ndiye Aliyepeleka Mtume kwa Al-Ummiyyiyna [watu wasioelewa kusoma wala kuandika] miongoni mwao anawasomea Aayah Zake na Anawatakasa, na Anawafunze Kitabu [Qur-aan] na Hikimah [Sunnah], na japo walikuwa kabla katika upotofu bayana))9 Fadhila za kusoma, kuhifadhi na kuisikiliza Qur-aan ni nyingi kama zilivyotajwa katika Qur-aan na Sunnah. Vitabu na makala nyingi zimeandikwa kuhusiana na hilo; zifuatazo ni baadhi ya fadhila zake • Kama biashara isiyofilisika: ZπuŠÏΡŸξtãuρ #uÅ öΝßγ≈uΖø%y—u‘ $£ϑÏΒ (#θà)xΡr&uρ nο4θn=¢Á9$# (#θãΒ$s%r&uρ «!$# |=≈tGÏ. šχθè=÷Gtƒ tÏ%©!$# ¨βÎ) ∩⊄∪ u‘θç7s? ©9 Zοt≈pgÏB šχθã_ötƒ ((Hakika wale wanaosoma Kitabu cha Allaah [Qur-aan], na wakasimamisha Swalaah, na wakatoa kutokana na yale Tuliyowaruzuku kwa siri na [kwa] dhahiri wanataraji tijara isiyofilisika)) 10 8Al-‘Imraan (3: 164) (62: 2) 10Faatwir (35: 29) 9Al-Jumu’ah 7 www.alhidaaya.com • Mbora Miongoni Mwa Waumini Bila shaka yoyote ile yenye ubora au uzuri wa kitu huthibiti kwa sababu hii au ile au kwa kufungamana na mwenye hicho kitu; na ubora au uzuri wa Qur-aan ni kwa kuwa ni Maneno ya Aliyembora kabisa; na kuna ubora gani ulimwengu huu kuliko mtu kujifunza au kufundisha Maneno ya Allaah; jambo alilolianza mwalimu aliyebora kuliko wote hapa duniani ambaye ni Mtume ( ). Hivyo hakuna kazi wala amali iliyobora kuliko ile kazi au amali aliyoifanya Mtume ( ) ambayo ni kusoma na kuisomesha Qur-aan kama ilivyothibiti katika Hadiyth: ((* + +$ , - . , / )) : ! " #$ % & ' ! Impokelewa kutoka kwa 'Uthmaan bin 'Affaan (0 123) kwamba Mtume ( ) amesema: ((Mbora wenu ni yule mwenye kujifunza Qur-aan kisha akaifundisha))11 • Thawabu Kwa Kila Herufi Moja: Kusoma au kusomesha Qur-aan ni ‘ibaadah kama ilivyotangulia; na ni ‘ibaadah yenye kumpatia mwenye kuabudu malipo makubwa kama itafungamana na sharti kubwa katika masharti ya ‘ibaadah katika Uislamu ambalo ni ikhlaasw. Hivyo mwenye kuisoma Qur-aan kwa nia safi huwa na matarajio ya malipo kama haya yaliyothibiti katika Hadiyth ya ibn Mas’uud (0 123) kwamba Mtume ( ) amesema: 55 5 + 5 5 5 <6 = #> 5#?. 6 5 @ $ 5A B0" 4 9 :; 4 56 - 75 8 4B0" 9 A ,C D#E - . #FC 9 6 ,< - . )) 5 4 9 = 8 ((8 4 9 4 . 8 4 4 9 ((Atakayesoma herufi moja katika kitabu cha Allaah atapata hasanah [jema] moja, na kila hasanah moja ni sawa na 11Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhy, An-Nasaaiy, Abu Daawuwd, Ahmad 8 www.alhidaaya.com thawabu kumi, wala sisemi 'Alif-Laam-Miym' ni herufi moja, bali Alif ni herufi moja na Laam ni herufi moja na Miym ni herufi moja))12 • Kuwa Miongoni Awapendao: Mwa Watu Wake Allaah (وتعالى )سبحانه Qur-aan kama tuaminivo ni Maneno ya Allaah, hivyo mwenye kushikamana nayo iwe kwa kuisoma na vyenginevyo huwa ni miongoni mwa watu Wake Allaah Anaowapenda. Imethibiti hili katika Hadiyth ifuatayo: 5 5 +5 5 $ ( * ! + , 5 0 - .5 - ((G#+ ) . H 6 + I)) : - ! 5 JH 6 H )) : ((E + #/ 5 + J H 6 0 ! * . $ 1 . Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maalik (0 123) kwamba Mtume ( ) amesema ((Allaah Anao watu wa aina mbili Anaowapenda katika watu)). Wakamuuliza, ee Mtume wa Allaah, ni nani hao? Akasema: ((Hao ni watu wa Qur-aan na ni watu wa Allaah Awapendao))13 • Thawabu Hata Kwa Mwenye Kuisoma Kwa Mashaka: Wengi huachana na kitu au jambo lolole lile khasa likiwa linahusiana na kusoma au kutafuta elimu ikiwa litakuwa lina taabu na mashaka ndani yake; isipokuwa kwa wenye moyo mgumu na subira isiyoelezeka au lengo analotaka kulifikia au malipo aliyoahidiwa kuyapata; kwa kuelewa hayo basi Mtume ( 2 3 ) hakutaka Waislamu wakate tamaa au waache mara moja kusoma au kujifunza kusoma Qur-aan kwa kisingizio kuwa lugha yenyewe kwanza mtu haielewi, pili hata akisoma huwa anadodosa dodosa na pengine watu kumcheka maana anasoma kwa mashaka na taabu kubwa; kwa kuelewa hayo Mtume ( ) aliwatia nguvu Waislamu kwa kuwahakikishia kuwa malipo yako kwa kila 12At-Tirimidhiy 13Ahmad, Ibn Maajah 9 www.alhidaaya.com msomaji wa Qur-aan hata kama anapata mashaka ikiwa ana ikhlaasw: 5K3,& 57 5 5 5 + L. $ 5 5 6 7 ! #5A H#* )) : K " . 4 5 M6 ON #P 5 ;H 5 C5 LE$ ,EE,Q 6 ,Q RS5 + (( Imepokelewa kutoka kwa 'Aaishah (#>0 123) kwamba Mtume ( ) amesema: ((Yule aliyekuwa hodari wa kusoma Qur-aan atakuwa pamoja na Malaika Waandishi wa Allaah, watukufu, wema. Na yule ambaye anaisoma Qur-aan kwa mashaka na huku anajitahidi kwa kudodosa atapata ujira mara mbili))14 • Harufu Nzuri Na Ladha Nzuri Kwa Anayeisoma Qur-aan: Mtume ( ) ametofautisha mfano wa Muumini anayesoma na asiyesoma Qur-aan katika Hadiyth iliyopokelewa toka kwa Abu Muwsaa Al-Ash'ariy(0 123) : 5 5 5 RS5 + -5 .5T * J ?. U 35 BM+ ,X J5 ?* 6 ,Q RS+ -5 .T * J ?. )) 4 V W #> * $ W U 4 V W #> Q 5 ((;4 9 #> * $ W #> YQ 35 = K *+ E J5 ?* 6 ,Q = Imepokelewa kutoka kwa ((Mfano wa Muumini ambaye anayesoma Qur-aan ni kama tunda la Utrujjah15; harufu yake nzuri na ladha yake nzuri. Na mfano wa Muumini asiyesoma Qur-aan mfano wake kama tende zisizokuwa na harufu lakini zina ladha tamu))16 14Al-Bukhaariy na Muslim linalofanana na ndimu lenye rangi ya orenji inayokaribia rangi ya dhahabu, linajulikana kama tufaha la ki-Ajemi. Lina harufu nzuri kabisa. 15Tunda 16Al-Bukhaariy, Muslim, Ahmad, An-Nasaaiy, Abu Daawuwd, Ibn Maajah 10 www.alhidaaya.com • Qur-aan Ni Kiombezi Siku Ya Qiyaamah: Mwenye kupenda kutafuta marafiki na maswahiba wa kweli na wakumfaa basi afanye usahiba na Qur-aan kwani haina kawaida ya kumtupa mkono swahiba wake wakati wa shida na fazaa: 9 :1 +%Z5C [ ,<)) :. $ 4; . "< 0 5 * * - 8- ! 5 5 5 5 ((5 5A# X #$ F P B.# ; ,Q 15\Q Imepokelewa kutoka kwa Abu Umaamah Al-Baahiliyy (0 123) ambaye amesema: “Nimemskia Mtume ( ) akisema: ((Someni Qur-aan kwani itakuja siku ya Qiyaamah ikimuombea aliyekuwa swahiba wake [mwenye kuisoma]))17 • Qur-aan Humnyanyua Mtu: 5 S >5A LC,Q + + 5I)) : 5 E7 L ] @ Q #.F ; ,<6 D# = % > * - ? & ((-Q 5 5A 5 / 'Umar (0 123) amesema: “Mtume wenu amesema: ((Allaah Atawanyanyua baadhi ya watu kwa kitabu hiki [Qur-aan] na Atawadhalilisha wengine kwa kitabu hiki))18 • Qur-aan Humpandisha Mtu Daraja Ya Pepo: 5 5 :# 5 U ^5 3 6 ,< ! ?( & ! + @ ! ,Q)) : 5 9#_ 5 c 0 5 ` ((#> 5A 6 , BeQ 5 / Ea5 0 . + Z5C # ,%cb 15C J V , d 0 #* J V3 Imepokelewa kutoka kwa 'Abdullaah bin 'Umar (#*>0 123) kwamba Mtume ( ) amesema: ((Huambiwa swahiba wa Qur-aan [aliyeshikamana na Qur-aan]: “Soma na panda [juu katika daraja za Pepo] na uisome kwa 'Tartiyl' 17 18 Muslim Muslim Ibn Maajah, Ahmad 11 www.alhidaaya.com [ipasavyo kwa tajwiyd] kama ulivyokuwa ukiisoma ulipokuwa duniani, kwani makazi yako ni pale utakapofika katika Aayah ya mwisho utakayoisoma))19 • Huteremka Malaika Kwa Utulivu Na Rahmah Kwa Wanaosoma Qur-aan: $ 5 ,A -.5 d e ,A 15C 4;,< L*EM f; A?:1?0 8- ! #. )) : . 5 5 > ,E + 9 B* 9 + > ,E @5 g B0 75 " + >5 d a ,% =+5I > ,0, ,A %; 3 c E,Q 5 + D# E ;,E ,Q + 5 5 ((hc 0 5 - * C + H i B7 j! * Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (0 123) kwamba Mtume ( ) amesema ((Hawakusanyiki pamoja watu katika miongoni mwa nyumba za Allaah wakisoma kitabu cha Allaah, na wanafundishana baina yao, ila huwateremkia utulivu na hufunikwa na Rahmah na Malaika huwazunguka na Allaah Anawataja mbele ya [Malaika] aliokuwa nao))20 L -?9 :I ,M?N J L -?9 :I , ?:I 4 J K > ,B@+? * C -?9 :1 5D : . 0 & ::+ E( F G ! + @ -4 - ! R I " -$ S . :I 5 <T U '* K VI R :> 4 .F D 1- 4 J & 9 :I W X YZ % - 4 6[ I" :@P - C 4 ."0 $ - * \ G .] '* J ? ^? _< @ a:I" : . $ ` $ 1 :4 9 :I 9 :I .""?:I 4 J K > b@+? * C -?:- U c. J ! * 5 G $ - & ::+ . $ 9 :I ."F ((e ] 9 - A 6 ,<)) : D 1- 4 J L ` -?9 :I" : . $ < ((e ] 9 :I ."F 9 - A 6 ,<)) : D 1- 4 J L ` -?9 :I" ::# . R :* D 1? W X % d 4 ((e ] $ 9 - A 6 ,<)) : I?e I" : . . C 4 $ 9 :I ."0 $ - * \ G .] '* - R I 5 <T U '* 4 J ? ^? _< 1-?:I ,BYZ % - 4 6N 19At-Tirmidhiy, 20 Abu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad Muslim Abu Daawuwd, Ibn Maajah , Ahmad 12 www.alhidaaya.com G#+ & %# B7 5j! * ` 6 ,< ; ` L *5 E" d 5)) : X f 0 #H ,Q d (( > ,0 .5 5EE" #. Imepokelewa kutoka kwa Usayd bin Khudhwayr, kwamba alipokuwa akisoma akiwa katika mirbad21 yake akashtuka farasi wake. Akasoma, kisha akashtuka tena, akasoma kisha akashtuka tena. Akasema Usayd: Nikaogopa asije kumkanyaga Yahya (mwanawe). Nikainuka kumwendea (farasi) nikaona kitu kama kivuli juu ya kichwa changu kama kina kandili kikipanda mbinguni hadi kikapotea. Nikamwendea Mtume ( ) siku ya pili nikwamwambia: “Ee Mjumbe wa Allaah. Jana usiku nilipokuwa katika mirbad yangu nikisoma Qur-aan, farasi wangu alishtuka! Mtume ( ) akasema: ((Soma Ibn Khudhwayr)). Akasema: Nilisoma lakini alishtuka tena. Mtume ( ) akasema: ((Soma Ibn Khudhwayr)). Akasema: Nilisoma lakini alishtuka tena. Mtume ( ) akasema ((Soma Ibn Khudhwayr)). Akasema niliondoka kwani Yahya alikuwa karibu naye, nikahofu asimkanyage. Nikaona kama kivuli kikiwa na taa kinapanda juu hadi kikapotea. Akasema Mtume ( ): ((Hao ni Malaika walikuwa wakikusikiliza, lau ungeliendelea kusoma hadi asubuhi watu wangelikiona kisingelipotea))22 • Kuhifadhi Na Kujifunza Maana Ya Qur-aan Ni Bora Kuliko Mapambo Ya Dunia: $ ^?N U 9 :I 5 fe < C ! g b 5 Q 7 bQ6)) : . ?( * ! + 5 9 ! e 5 5 $ 5I 6 # L5 k< = e m5I 5 g 15C -5 Q# .; -5 ,E,<#05A 0 .5 1 5\ ,C ^ kA 5I ; ,Q J+ c l,Q 6 < g . 6 ,Q 6 $ , ,C c5 n5 " * 5I c 9 ) $ 1 9 :I ((e 953 K h 6 c l,Q ! C6)) : 5 5 5 E5 -.5 -5 ,E,Q e !m -.5 , / o - .5 4 , / L4 A3 6 o 4 4 !m -5 ,E,<#% - . 4 , / J+ M a+ + D# 5 - .5 -+ H5 q5 c 6 - .5 Le A3 6 ((J5 5Ap 21 22 Sehemu ya mifugo ya farasi Al-Bukhaariy, Muslim 13 www.alhidaaya.com Imepokelewa toka kwa 'Uqbah bin 'Aamir (0 123) ambaye amesema: “Mtume ( ) alitujia wakati tulikuwa katika Swuffah23 akauliza: ((Kuna yeyote miongoni mwenu anayetaka kwenda soko la Butw-haan24 au [soko] la Al'Aqiyq25 na akapata humo ngamia wawili wakubwa na waliyonona bila ya kutenda dhambi au kukata undugu?)) Tukajibu kwamba sote tunapenda kufanya na kupata hivyo. Kisha akasema: ((Basi aende mmoja wenu msikitini akajifunze au asome Aayah mbili katika kitabu cha Allaah عزوجلbasi akifanya hivyo ni bora kuliko ngamia wawili. Na Aayah tatu ni bora kuliko ngamia watatu, na Aayah nne ni bora kuliko ngamia wanne, na mfano wa hivyo hivyo wa Aayah kwa ngamia))26 • Mwenye Kuhifadhi Qur-aan Huvalishwa Taji Siku Ya Qiyaamah: D , ,C B5 .# 5 ; ,Q [1n5 Q)) : V 3 #Q :; ! A?:1?0 8- ! 5V 5 V 3 #Q ::; u ,Q + m B5 . 7 B+9 s ,Q + m B5 . 7 r# V 3 #Q ::; 3 D s &, ,C ,hq t D &, ,C ,9 e 5 a , .O 3 6,< : :# ((FB0" , ,C 0 2 , ,C 0 9 BQ JV 7 A q Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (0 123) kwamba, Mtume ( ) amesema: ((Qur-aan itakuja siku ya Qiyaamah na itasema: “Ee Mola, Mpambe” [Mwenye kuhifadhi Qur-aan]. Kisha atavalishwa taji. Kisha [Qur-aan] itasema: “Ee Mola, muongeze”. Kisha huyo mtu atavishwa nguo ya heshim. Kisha itasema: “Ee Mola Ridhika naye”. Allaah, Ataridhika naye. Kisha ataambiwa: “Soma na panda”. 23 Sehemu katika Msikiti wa Mtume ( 2 3 ) waliyokuwa wakikaa Maswahaba ambao hali zao walikuwa ni masikini. 24 Bonde lilioko Kusini mwa mji wa Madiyna kuelekea upande wa Magharibi karibu na Jabali la Sal’. Mtume ( 2 3 ) alitawadha katika bonde hili siku ya vita vya Khandaq 25 Bonde maarufu kabisa katika mjia wa Madiyna au eneo la Al-Hijaaz yote. Liko umbali wa maili kilometa mia Kusini na linaelekea upande wa Mashariki. Linajulikana kuwa ni ‘Bonde lenye Baraka’. 26Muslim, Abu Daawuwd, Ahmad 14 www.alhidaaya.com Atapokea thawabu [atakayosoma]))27 zaidi ya mema kwa kila Aayah • Mwenye Qur-aan Zaidi Huwa Na Mwanga Kaburini: J? j:+ k&l % d . @( G $ % - @ ! + ?+J ! - :i: ! * j - > Ep - KVI (( m 5 5 SF / 6 ,? 6 #*>,bQ6)) :. ( @ C * 9 :1 L @( G @ o@G . :n C Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (0 123) kwamba alikuwa Mtume ( ) akiwakusanya watu wawili waliokufa katika vita vya Uhud katika nguo moja kisha anauliza, ((Nani katika hao mwenye ujuzi zaidi wa Qur-aan?)) Anapojulishwa mmoja kati ya hao, humtanguliza 28 mwanandani)) 27At-Tirmidhy na Al-Haakim An Nasaaiy 28Al-Bukhaariy, 15 www.alhidaaya.com 04-Umri Bora Wa Kuhifadhi Qur-aan Umri mzuri utakaofanya sahali kuihifadhi Qur-aan ni baina ya miaka mitano hadi ishirini na tatu; bali ni bora zaidi kuihifadhi utotoni kabla ya kufikia umri wa kubaleghe, kwani wakati huo vijana hushughulishwa na dunia, hasa zama hizi zilizojaa fitnah huwa si wepesi kuepukana nazo ila tu kwa Rahma ya Allaah ()سبحانه وتعالى. Anapokuwa angali mtoto, kuhifadhi chochote kichwani huwa ni sahali kwa sababu bongo huwa na kumbukumbu nzuri bado na si wepesi kusahau anachokihifadhi. Imesemekana kwamba: 5 ,+0# 5 &75 15C 5 ,+0# 5 l_ "[5 #* v 5 w5 n v 5 " V 15C "Kuhifadhi29 udogoni ni kama nakshi katika jiwe, na kuhifadhi ukubwani ni kama nakshi katika maji. Ina maana: Kuchonga au kuchora nakshi katika udongo uliomaji, mchoro huo hubakia milele kuwa ni alama katika jiwe litakapokauka. Ama mwenye kuchora katika maji, mchoro huo hutoweka. Hata hivyo, haimaanishi kwamba aliyefikia umri mkubwa haitowezekana kwake kuihifadhi Qur-aan, bali mtu anapopendelea kutekeleza ‘amali hii tukufu, ajitahidi na Allaah ()سبحانه وتعالى Atamfanyia sahali kwa sababu ahadi ya Allaah ( )سبحانه وتعالىkatika Suwratul-Qamar haikutofautisha kati ya mtoto au mtu mzima. Wako walioihifadhi Qur-aan wakiwa na umri zaidi ya miaka arubaini. Bali imesemekana kwamba mtu aliyefikia miaka zaidi ya sabiini aliweza kuihifadhi Qur-aan. Muislamu anapaswa awe na iymaan na yakini kuhusu maneno ya Allaah ( )سبحانه وتعالىna kuwa na dhana njema, matumaini na matarajio mazuri daima. Kufanya hivyo, itakupa nguvu ya azimio la kuihifadhi Qur-aan. Hivyo ni fursa tukufu kwa Muislamu kuhifadhi Qur-aan. Lakini ikiwa fursa hii imekupita na sasa inaelekea kwamba huna uwezo wa kuhifadhi Qur-aan, basi fanya hima na juhudi kuwahifadhisha watoto wako wakiume na wakike. Usiache fursa hii ikawapita wao pia kwani furaha yao ya kuhifadhi Qur-aan itakuwa ni furaha na 29 Kauli nyingine imetaja ‘Elimu udogoni ….’ 16 www.alhidaaya.com fakhari kwako na kupata Radhi za Allaah ( )سبحانه وتعالىna utakuwa umeshajitangulizia Aakhera akiba. 05- Nasaha Za Kuhifadhi Qur-aan Kabla ya kuanza kuhifadhi Qur-aan jitayarishe kutekeleza nasaha zifautazo: • Kutia Niyya Safi (Ikhlaasw) Anza na kutia niyyah ya dhati kwamba unakusudia kuhifadhi Qur-aan kwa ajili ya kupata Radhi za Allaah ( )سبحانه وتعالىna kutegemea fadhila na malipo yake, na hivi ndivyo inavyopasa katika ‘ibaada na amali zote. • Azimio la nguvu bila ya kukata tamaa. Weka azimio la nguvu, usichoke, usikate tamaa wala usivunjike moyo hasa pale utakapoona kwamba unazorota katika baadhi ya Aayah au Suwrah utakazoziona ngumu. Chukua mfano wa anayetaka kupanda mlima, akaupanda pole pole hadi kufikia kileleni. Hivyo basi japokuwa utakuwa unahifadhi kidogo kidogo, endelea usiache na kumbuka kauli ya Mtume ()صلى ﷲ عليه وآله وسلم: qfi* 5 5 q#. 5 5I -5 QVc U ((&9# + 9 6 # ,;b* +E9 + Jb * Q = ...)) (…Allaah Hachoki [kulipa thawabu] mpaka mchoke wenyewe. Na ‘Ibaadah Aipendayo zaidi ni ile inayodumishwa na mtendaji)).30 • Kuomba du'aa Muombe Allaah ( )سبحانه وتعالىAkupe tawfiyq ya kuhifadhi maneno Yake. Usiache kuomba kila mara. Tumia Wasiylah31 na nyakati za kukubaliwa du'aa. 30 31 Al-Bukhaariy na Muslim. Kuikurubisha kwa Allaah ( ) kwa ‘ibaadah 17 www.alhidaaya.com • Tambua Fadhila za kusoma na kuhifadhi Qur-aan Soma fadhila hizo upate hima ya kuzichuma na ikupe azimio la nguvu. • Kubakia katika Taqwa Anasema Allaah ()سبحانه وتعالى: 〈 3 ª!$# ãΝà6ßϑÏk=yèãƒuρ ( ©!$# (#θà)¨?$#uρ ((Na mcheni Allaah, na Allaah Anakufunzen))32 Kwa hiyo jisafishe kwanza na madhambi kwa kuomba maghfirah na kutubia kwa Allaah ()سبحانه وتعالى, kisha jiepushe na maasi yote kwani maasi yanamzuia mja kushika maneno ya Allaah ()سبحانه وتعالى. Ibn Mas-‘uwd ( )رضي ﷲ عنهamesema: 5 5 QU & _ e %S 5A $ J M + +5I "Hakika mtu anazozitenda" hunyimwa elimu kwa dhambi Imaam Ash-Shaafi'iy ( )رحمه ﷲalikuwa mwepesi wa kuhifadhi Qur-aan lakini Qur-aan ilipokuwa nzito kuihifadhi alisema: 5 5 Le 5 I f 5 5 5 5 5 ; 7 P z , I 1%c P 3\ C ,1y 9 [; $ + \A 1% ,&/ 6 . 1#$* 5 $5 {c > ,Q = 5 3;% ,3;% 1# 4 "Nililalamika kwa Wakiy’i kuhusu kushindwa kuhifadhi Qur-aan akaninasihi kuacha maasi na akanijulisha kuwa nuru ya elimu na nuru ya Allaah haimfikii mwenye kuasi" • Kutoshughulika na anasa za dunia 32 Al-Baqarah (2: 282) 18 www.alhidaaya.com Inampasa mwenye kutaka kuhifadhi Qur-aan atumie muda wake wote kwa ajili ya kuhifahdi Qur-aan. Ajitenge na anasa za dunia asizichanganye na kazi hii, ili akili na moyo wake upate utulivu kwa ajili ya hifdhwul-Qur-aan. Watu hupoteza wakati wao mwingi kushughulika na mambo ya upuuzi yasiyomzidishia Iymaan wala kumfaa Akhera yake. Fitnah zimekuwa nyingi na nyenzo zake zimekithiri; mitandao, televisheni, simu za mkono na huduma zake n.k. Wengineo hukaa mabarazani kwa maongezi au michezo ya karata n.k. Anayechanganya anasa, upuuzi n.k. na huku akitaka kuhifadhi Qur-aan hatoweza kabisa kwani Anasema Allaah ()سبحانه وتعالى: 〈 4 µÏ ùÏ θö _ y ’ûÎ É ÷ 7t =ù %s ΒiÏ ≅ 9 _ ã t 9Ï ! ª #$ ≅ Ÿ èy _ y $Β¨ Allaah Hakujaalia mtu yeyote nyoyo mbili kifuani mwake33 • Kuipa Hifdhwul-Qur-aan Kiupambele Katika ratiba za siku maishani mwako, lazima uipe hifdhwulQur-aan kiupambele. Jiwekee wakati maalumu kila siku uwe kwa ajili ya kuhifadhi Qur-aan tu. Wakati bora kabisa uliotambulika kuwa ni muwafaka kuihifadhi Qur-aan ni nyakati za usiku ambako kuna ukimya na utulivu. Bali wakati mzuri kabisa ni kabla ya Alfajiri au baada ya kuswali tu Alfajiri kwa sababu hapo bongo bado liko freshi na liko tayari kupokea na kuhifadhi kinachosomwa. Hilo limetambulikana kutokana na uzeofu wa waliohifadhi Qur-aan na jambo hilo halina shaka kwani kulingana na mchana, ni tofauti kabisa kwa sababu mchana kuna harakati nyingi ambazo zinaweza kukukatiza hifdhw yako; mfano watu ingia toka, simu n.k. • Jifunze Kwanza Kuisoma Qur-aan Bila Ya Makosa Inapasa mwenye kutaka kuhifadhi Qur-aan kwanza ajifunze kuisoma Qur-aan sawa sawa bila ya makosa kwani unapohifadhi kosa huwa vigumu baadaye kulirekebisha. Juu 33 Al-Ahzaab: (33: 4) 19 www.alhidaaya.com ya hivyo kuisoma Qur-aan kimakosa hubadilisha na kupotosha kauli za Allaah ()سبحانه وتعالى.34 • Jifunze Kuisoma Qur-aan Kwa Hukmu Za Tajwiyd Kusoma kwa kufuata hukmu za Tajwiyd husaidia kutambua maneno yanayofuatia, mfano baada ya maddum-munfaswil (madd ya kuachana) utajua tu kwamba neno la pili litakuwa linaanzia na herufi ya hamza. Vile vile unapojifunza Tajwiyd ndipo utakapoweza kuisoma Qur-aan kwa kuitamka vizuri ipasavyo na kuvuta panapotakiwa na kufanya ghunnah35 panapotakiwa n.k na ndipo qiraa-a cha mtu kinapokuwa kizuri. • Jifunze Lugha Ya Kiarabu Muislamu anapaswa kujifunza lugha ya Kiarabu aweze kufahamu maneno ya Mola wake. Lugha ya Kiarabu itamsadia pia mwenye kuhifadhi Qur-aan kutambua vipi kutamka neno linaloanzia au linalofuatia kwa vile maneno hubadilika kutokana na hukmu za serufi ya lugha ya Kiarabu.36 Waislamu wengi hawatilii hima kujifunza lugha hii tukufu. Baadhi ya watu wako tayari kulipia gharama kubwa ya kujifunza lugha nyinginezo na hali lugha ya Kiarabu ndio iliyowajibika kwanza ili kuweza kufahamu maneno ya Allaah ( )سبحانه وتعالىna ya Mtume Wake ()صلى ﷲ عليه وآله وسلم. • Tumia Aina Moja Ya Mswahafu Tumia Mswahafu wa aina moja, usichanganye miswahafu katika kuhifadh kwa sababu mpangilio wa Suwrah zinavyoanza na kumalizikia zinatofautiana katika baadhi ya miswahafu, na hivyo hata Ayaah huwa zimetofautiana katika kupangika kwake kwenye ukurasa. Utakuta katika aina ya Mswahafu mmoja Aayah fulani imeanzia juu ya ukurasa, lakini Aayah hiyo hiyo katika aina nyingine ya Mswahafu Rejea kitabu cha: Alhidaayah Katika Ahkaam Za Tajwiyd- Mlango wa ‘Makosa Ya Dhahiri Na Yaliyofichika’ 35 Sauti inayaotokea puani 34 20 www.alhidaaya.com imepangika katikati au chini ya ukurasa. Kutumia aina mbili za mswahafu kutambabaisha mwenye kuhifadhi kwa sababu mtu anapohifadhi Aayah huwa ni kama taswira (picha) iliyotua akilini na kubakia katika kumbukumbu. Ndio maana utamuona aliyehifadhi Qur-aan huwa ni sahali kwake kutambua Aayah iko sehemu gani ya ukurasa. • Sikiliza Ulichohifadhi Kila Mara Mchague Qaariu (msomaji) unayependa kumsikiza urudie kuzisikiliza Aayah ulokwishazihifadhi hadi zithibitike moyoni. Ni neema za Allaah ( )سبحانه وتعالىkwamba imekuwa sahali mno zama hizi za maendeleo ya teknologia, kupata visaidizi mbali mbali vya kumsaidia mwanafuzi katika mafunzo ya Dini yake tena bila ya gharama kubwa. • Vyakula Na Miti Shamba Ya Kusaidia Kumbukumbu Imetambulikana kuwa baadhi ya vyakula au miti shamba husaidia ubongo kuamsha kumbukumbu na kutibu usahaulifu. Tumia vyakula na miti shamba ifuatayo upate natija nzuri In Shaa Allaah: Asali, habbat-sawdaa (haba soda), lozi, tende, majani ya jarjiyr, zabibu, mafuta ya zaytuni au zaytuni zenyewe, tiyn, lubaan-adhikr (ubani wa kumbukumbu au ubani wa maji), nanaa (weka katika chai ukipenda), zaatari, tangawizi, 'arqisus (vijiti fulani vya mitishamba vinaponyesha kifua pia). Michanganyiko ifuatayo Imetambulikana kuleta manufaa: • Saga njugu za pistachio, zabibu nyeusi, lozi, lubaan-adhikr kisha tia katika asali kiasi cha kuchanganyika vitu vyote hivyo vizuri na kula asubuhi na jioni kijiko kimoja cha chai. • Loanisha nyuzi chache za zaafarani katika maziwa ya dafudafu, subiri ilowanike kisha kunywa. 21 www.alhidaaya.com 06- Utaratibu Wa Kuhifadhia Qur-aan Kuhifadhi Qur-aan inategemea uwezo wa mtu; kuna wanaoweza kuhifadhi ukurasa mmoja kwa dakika chache tu. Wengineo huwachukua masaa. Kulingana na uwezo wako, fuatilia utataribu ufuatao unaotumika zaidi kwa kuwa umeonekana ni muwafaka na unaoleta najita nzuri. • Soma Aayah unazotaka kuhifadhi uhakikishe unazisoma sawa sawa bila ya makosa yoyote. • Anza kuhifadhi Aayah moja, ikithibitika moyoni, isome mara kumi. • Ongeza Aayah ya pili ikithibitika soma mara kumi, kisha rudia Aayah ya mwanzo na hii ya pili usome mara kumi zote mbili. • Ongeza Aayah ya tatu uhifadhi, ikithibitika, isome mara kumi, kisha rudi kuanzia Aayah ya mwanzo, ya pili na hii ya tatu usome mara kumi zote. Endelea hivyo hivyo kwa kadiri ya uwezo wako wa kuhifadhi kwa siku kama ni Aayah tatu utakomea hapo, kama una uwezo wa kuhifadhi zaidi utaendelea kwa utaratibu huo huo. • Usiendelee mbele hadi uwe umezithibitisha Aayah ulizozihifadhi vizuri. Ukifanya kosa urudie kuihifadhi Aayah yenye kosa hadi kusikuweko na makosa kabisa. Hatimaye Utakapoweza kuhifadhi ukurasa mzima, usikilizwe na pindi ukikosea makosa zaidi ya matatu basi urudie kuzihifadhi tena ukurasa huo mpaka uthibitike. Utaratibu huu wa kurudia tokea Aayah za mwanzo na kuzirudia kusoma mara kumi husaidia kukumbuka mfuatano wa Aayah bila ya kuipita moja katikati. 22 www.alhidaaya.com • Ikiwa unajihifadhisha mwenyewe, ni muhimu upate mtu akusikilize kila unapothibitisha moyoni Aayah kadhaa akusikilize pia unapofanya marejeo ya hifdhw ya Suwrah ulizozihifadhi. • Soma kwa sauti ya kusikilizika na sio kimya kimya. Ukiwa ni peke yako, jifungie chumbani uwe huru kuisoma kwa sauti ya juu. • Siku ya pili, endelea kuchukua Aayah mpya kadiri uwezavyo. Zihifadhi kwa utaratibu huo huo. • Utakapomaliza, fanya marejeo ya kuzisoma Aayah ulizohifadhi mwanzo yaani jana yake, kisha unganisha na hizi mpya hadi zote zithibitike moyoni. • Siku ya tatu endelea hivyo hivyo, kila unapozidi kuhifadhi ndipo unapozidi kupanua ubongo wako kuweza kuhazini Aayah nyingi akilini lakini pia ndipo kila unapohitaji muda wa kurudia Aayah za mwanzo ulizozihifadhi. • Kuziandika Aayah katika kitabu au ubao ni njia mojawapo iliyojaribiwa na kuonenakana imeleta natija ya kusaidia hifdhw ya Qur-aan. 23 www.alhidaaya.com 07-Zingatia Aayah Zinazofanana Anasema Allaah ()سبحانه وتعالى: 〈’ u ΤÎ $Ws Β¨ $γ Y 6Î ≈± t Ft Β• $6Y ≈Gt .Ï ] Ï ƒ‰ Ï tp :ø #$ z ¡ | m ô &r Α t “¨ Ρt ! ª #$ Allaah Ameteremsha kauli nzuri kabisa; Kitabu (Qur-aan) zinazoshabihiana (kauli zake kwa uzuri na haki bila kupingana na) zenye kukaririwa kila mara (bila ya kuchosha)37 Anayehifadhi Qur-aan aghalau hutatizwa na kubabaika katika Aayah zinazofanana katika Qur-aan. Kufanana kwake huwa ima kwa kutangulia neno au maneno, au kutofautiana katika herufi au irabu n.k. Utakapozitambua na kuzihifadhi sawa sawa kauli hizo, basi utajiepusha na kutatizwa huko In-Shaa-Allaah. Kuna vitabu kwa lugha ya Kiarabu ambavyo vimetaja Aayah hizo laiti kama vingefasiriwa vitabu hivyo kwa lugha ya Kiswahili. Mifano michache ya kauli za Allaah ( )سبحانه وتعالىzinazofanana ni kama ifautavyo: • Mfano wa kwanza: ( «!$# Îö&tóÏ9 ϵÎ/ ¨≅Ïδé& !$tΒuρ ... … Wa maa uhilla bihi lighayri-LLaah38 Aayah hii katika Suwratul Baqarah ni pekee iliyotanguliza neno la ‘bihi’ kabla ya ‘lighayri-LLaah’ : Ama kwengineko kama katika Suwratul-Maaidah (5:3) Suwratul-An-aam (6: 145) Suwratun-Nahl (16:115) imekuwa tofauti na hiyo Aayah ya Suwratul-Baqarah kwa kuwa neno la ‘bihi’ limekuja baada ya ‘lighayri-LLaah’ . ( ϵÎ/ «!$# Îö&tóÏ9 ¨≅Ïδé& !$tΒuρ Wa maa uhilla lighayri-LLaah bihi 37 38 Az-Zumar (39: 23) Al-Baqarah (2: 173) 24 www.alhidaaya.com Pia katika Suwratun-Nahl haikuanzia na: $! Βt ρu . • Mfano wa pili: Zingatia kauli za Allaah ( )سبحانه وتعالىzifuatazo jinsi zilivyofanana na kutofautiana: $oÿÏ3 y7Ï9≡sŒ 3 Èd,y⇔ø9$# Îö&tóÎ/ z↵ÍhŠÎ;¨Ψ9$# šχθè=çGø)tƒuρ «!$# ÏM≈tƒ$t↔Î/ šχρãàõ3tƒ (#θçΡ%x. óΟßγ¯Ρr'Î/ y7Ï9≡sŒ ∩∉⊇∪ šχρ߉tF÷ètƒ (#θçΡ$Ÿ2¨ρ (#θ|Átã Dhaalika biannahum kaanuw yakfuruwna bi-aayaati-LLaahi wa yaqtuluwnan-nabiyyiina bighayril-haqq. Dhaalika bimaa ‘aswaw wa kaanuw ya’taduwn39 $yϑÎ/ y7Ï9≡sŒ 4 9d,ym Îö&tóÎ/ u!$uŠÎ;/ΡF{$# tβθè=çGø)tƒuρ «!$# ÏM≈tƒ$t↔Î/ tβρãàõ3tƒ (#θçΡ%x. öΝßγ¯Ρr'Î/ šÏ9≡sŒ ∩⊇⊇⊄∪ tβρ߉tG÷ètƒ (#θçΡ%x.¨ρ (#θ|Átã Dhaalika biannahum kaanuw yakfuruwna bi-Aayati-LLaahi wa yaqtuluwnal-anbiyaa-a bighayri haqq. Dhaalika bimaa ‘aswaw wa kaanuw ya’taduwn40 Kauli zifuatazo zimefanana lakini zimetofautiana katika irabu; ya kwanza imetajwa kwa fat-haa na pili kwa kasra. ãΝßγn=÷Fs%uρ (#θä9$s% $tΒ Ü=çGõ3oΨy™ ¢ â!$u‹ÏΖøîr& ßøtΥ w uρ ×&É)sù ©!$# ¨βÎ) (#þθä9$s% šÏ%©!$# tΑöθs% ª!$# yìÏϑy™ ô‰s)©9 9d,ym Îö&tóÎ/ u!$uŠÎ;/ΡF{$# …Waqatlahumul-anbiyaa41 39 40 41 Al-Baqrah (2: 61) Aal-‘Imraan (3: 112) Aal-‘Imraan (3: 181) 25 www.alhidaaya.com 9d,ym Îö&tóÎ/ u!$uŠÎ;/ΡF{$# ãΝÎγÎ=÷Fs%uρ «!$# ÏM≈tƒ$t↔Î/ ΝÏδÌøä.uρ óΟßγs)≈sV‹ÏiΒ ΝÍκÅÕø)tΡ $yϑÎ6sù …Wa qatlihimul-anbiyaa42 • Mfano wa tatu: Aayah zilofanana na kutofautiana kidogo katika kauli ya Allaah ( ) kuhusu Nabii Zakariyyah (rs_ ) na Maryam mama wa Nabii ‘Iysaa (rs_ ) katika Suwratul-’Imraan: ã≅yèøtƒ ª!$# šÏ9≡x‹x. tΑ$s% ( ÖÏ%$tã ’ÎAr&tøΒ$#uρ çy9Å6ø9$# zÍ_tón=t/ ô‰s%uρ ÖΝ≈n=äî ’Í< ãβθä3tƒ 4’¯Τr& Éb>u‘ tΑ$s% â!$t±o„ $tΒ … kadhaalika-Allaahu Yaf-'alu …..43 4 â!$t±o„ $tΒ ß,è=÷‚tƒ ª!$# Å7Ï9≡x‹Ÿ2 tΑ$s% ( ×|³o0 Í_ó¡|¡ôϑtƒ óΟs9uρ Ó$s!uρ ’Í< ãβθä3tƒ 4’¯Τr& Éb>u‘ ôMs9$s% … kaadhaliki-LLaahu Yakhluqu …. • Mfano wa nne: 9≅sWtΒ Èe≅ä. ÏΒ Èβ#uöà)ø9$# #x‹≈yδ ’Îû Ĩ$¨Ζ=Ï9 $oΨøù§|À ô‰s)s9uρ … lin-naasi fiy haadhal-Qur-aan…44 Hapa tunaona kwamba neno lin-naasi limetangulia. Ama katika Aayah ifuatayo limekuja baadaye. 4 9≅sWtΒ Èe≅à2 ÏΒ Ä¨$¨Ζ=Ï9 Èβ#uöà)ø9$# #x‹≈yδ ’Îû $oΨøù§|À ô‰s)s9uρ 42 43 44 An-Nisaa (4: 155) Aal-‘Imraan (3: 40) Al-Israa (17: 89) 26 www.alhidaaya.com … fiy haadhal-Qur-aan lin-naasi Mifano mingi mno imo katika Qur-aan iliyokuwa katika hali kama hizo, na vinginevyo. Na pia nyingi hutofautiana pale inapomalizika Aayah; mfano Aayah mbili zinazofuatiana katika Suwratul-Maaidah: ∩∉⊄∪ tβθè=yϑ÷ètƒ (#θçΡ%x. $tΒ š[ø⁄Î6s9 Labi-isa maa kaanuw ya’maluwn45 ∩∉⊂∪ tβθãèoΨóÁtƒ (#θçΡ%x. $tΒ š[ø⁄Î6s9 Labi-isa maa kaanuw yaswna'uwn46 Kisha katika Aayah Namba 79 imetofautiana tena: ∩∠∪ šχθè=yèøtƒ (#θçΡ$Ÿ2 $tΒ š[ø⁄Î6s9 Labi-isa maa kaanuw yaf'aluwn47 Zingatia pia Asmaa na Swifaat za Allaah ( ) zinavyomalizika ambazo mara nyingi zimetajwa mbili mbili, huwa zinatofautiana mara kwa mara. Asmaa na Swifaat za Allaah ( ) zimekariri zaidi katika Suwratun-Nisaa. Pia aina za adhabu zinavvyotajwa mwishoni mwa Aayah. Almuradi darsa hili ni pana mno inahitaji mijalada ya vitabu! Inatosheleza kwamba anayehifadhi Qur-aan atambue swala hii na awe makini mwenyewe katika kutambua kauli na maneno hayo. 45 46 47 Al-Maaidah (5: 62) Al-Maaidah (5: 63) Al-Maaidah (5: 79 27 www.alhidaaya.com 08-Kuithibitisha Qur-aan Baada Ya Kuihifadhi Kuhifadhi Qur-aan si tatizo kama kuithibitisha, kwa sababu mtu anaweza kuhifadhi ukurasa mmoja chini ya nusu saa, lakini ikiwa hakuifanyia juhudi kukariri kuisoma hadi ithibitike vyema moyoni, basi hapo itakuwa ni khasara kubwa kwa kuwa amepoteza juhudi kubwa na muda wingi kwa jambo ambalo mwishowe halikuthibiti lengo lake. Nasaha zifuatazo zitakusaidia kuithibitisha hifdhw yako In Shaa Allaah: • Dumisha kusoma Qur-aan Inakupasa ndugu uliyeihifadhi Qur-aan uendelee kuisoma Qur-aan kila siku, kila mara bila ya kuiacha. Kila siku uweke muda maalumu uwe khasa kwa ajili ya kuisoma Qur-aan na isiwe chini ya nusu juzuu kila siku! Na ukiweza kuisoma zaidi ndivyo utakavyoweza kuithibitisha zaidi. Ipe ratiba hii kipambele katika kila siku ya maisha yako. Tahadhari kauli zifautazo z Mtume ( 2 3 ) mojawapo aliyoiapia: RS5 +; ,C S H c H# $ ,)) ! . * 8- ! 5 - .5 #FEb , cb P 6 ; > 5hc5 5A ce *+ . s ,% ((#> 5 15C J5 5Ap Imepokelewa toka kwa Abu Muwsaa ( 3 "#$): Amesema Mtume ( 2 3 ): ((Dumisheni kuisoma Qur-aan. Naapa kwa Ambaye nafsi ya Muhammad imo Mikononi Mwake, hiyo (Qur-aan) ni wepesi kukimbia kuliko ngamia anavyochopoka katika kamba yake))48 J ?. #* +%5I)) #> W6 5I 48 $ % - &R: "# $ ?& ! + ! : . 5 J5 ?* 5 5 5 U 5 9# 5 9# #> 7 " 5I B5 + $ * J5 5Ap U . 6 #> , c H# ((d &H i Al-Bukhaariy na Muslim 28 www.alhidaaya.com Imepokelewa toka kwa ibn ‘Umar (&R 3 "#$) kwamba Mtume ( 2 3) amesema: ((Hakika mfano wa aliyehifadhi Qur-aan ni kama ngamia aliyefungwa, akimfunga atamzuia, na akimuacha ataenda zake))49 • Kabla ya kulala rudia Aayah ulizozihifadhi Imejaribiwa na kuonekana kwamba inasaidia kuthibitisha hifdhw ya Qur-aan kuzisoma Aayah uilizozihifadhi kabla ya kulala. Bali ni amali bora kabisa kwamba unasoma Qur-aan kabla ya kulala kwani huenda ikawa ndio amali yako ya mwisho pindi umeandikiwa kufariki usingizini ukajaaliwa husnulkhaatimah (mwisho mwema) na hivyo ndivyo itakavyokuwa hali ya kufufuliwa kwako. • Zisome Aayah ulizozihifadhi katika Swalaah za Sunnah. Hii ni njia bora kabisa ya kuthibitisha hifdhw yako. Zitume kwanza Aayah zilizothibitika vizuri moyoni, kisha pole pole ongezea nyinginezo. Inaruhusiwa kutumia Mswahafu katika Swalaah za Sunnah, kwa hiyo weka Mswahafu katika rafu ndefu inayofikia urefu wa mabega yako uweze kuisoma Quraan bila ya kuishika, na pale unapotatizwa na Aayah, upige jicho kuhakikisha na kujirekebisha. • Sikiliza Suwrah ulizozihifadhi. Pia ni njia nyingineyo muwafaka kabisa ya kuithibitisha hifdhw ya Qur-aan. Isikilize kila wakati kila mahali, kila unapopata fursa. Sikiliza hata unapokuwa unafanya kazi zako nyinginezo ingawa inalotakiwa ni kuisikiliza kwa umakini. Imesemekana kwamba baadhi ya watu wameweza kuihifadhi Qur-aan kwa kuisikiliza tu. Kuisikiliza Qur-aan itakusaidia pia kujirekebisha makosa yako na pia utakapomchagua Qaariu mwenye sauti nzuri inayekupendezea, utaweza nawe kuisoma kwa sauti hiyo hiyo. . • Ifundishe Qur-aan 49 Al-Bukhaariy na Muslim 29 www.alhidaaya.com Kazi hii humsaidia sana mtu kuithibitsha hifdhw yake. Je, kuna kazi bora zaidi ya kujifunza na kufundisha Qur-aan? Amesema Mtume ( 2 3 ) katika Hadiyth ya 'Uthmaan bin 'Affaan ( 3 "#$): ((* + +$ - . / )) ((Mbora wenu ni yule mwenye kujifunza Qur-aan kisha akaifundisha))50 50 Al-Bukhaariy 30 www.alhidaaya.com 09-Hitimisho: Tunamuomba Allaah ( )سبحانه وتعالىAtufanyie sahali katika amali hii tukufu na Atupe tawfiyq ya kuisoma kwa njia inayomridhisha Yeye Pekee, na Atuwezeshe kuihifadhi katika vifua vyetu na kuifanyia kazi maamrisho na makatazo yake na Atutakabalie du’aa zetu zote na khasa zifuatazo: 5 *H D#Hi #05%a96 [! M #%35c 3;% w#05A;,< L, 5A3 y5 $ J5 $M + >+ #0.; 5 *g 5 #5A #0*93 + > + .#0.; #% Vi + > + .FB* 9 3 {cF H 3; Q5 5 7 F % #.#F . 5I #0 $ M 5 5 5 5 FBn+ 9 #0 $ M 35 #> ,+0 [# % J5 + [# % ! #0,<t3 #0>5 M #. 0 . #0* V #0 "% #. 0 . 5 .- + 3 #Q *#$ D 5 5 5+ 5 15C #0 Q + |/ ` H 6 H -Q + > + .`E + > + S J5 H6 - . #0$ M 5 7 J5 $ M 5 _ 5 5 ,F# 5C3 B5 +0n I ,F#$ 5 P B5 .# 5 15C ,F3;% } V F#"%T . 5 & 1C ,#F0Q5 < # %cb 5 5 , ~ 5I ,F#A#n95 FE 5 35 #+0 -.5 5A F#.#. 5I F! 5q #> V f 5] 6 #Q z q;M ` 5 . F 5? F#* 5" + 5 5A# 5 ce *+ . #0V 5&% + J+ .- . X Ee Allaah Ijaaliye Qur-aan tukufu kuwa ni raha na uchanuzi wa nyoyo zetu, na nuru ya vifua vyetu, na utatuzi wa huzuni zetu, na sababu ya kuondoka wahka na dhiki zetu. Ee Allaah, turehemu kwa Qur-aan na ijaalie iwe ni kiongozi, nuru, Hidaaya na Rahma. Ee Allaah tukumbushe tunayoyasahu humo, na tufunze tuliyokuwa hatuayajui, na turuzuku kuisoma usiku na mchana na ijaalie iwe hoja yetu (isiwe hoja dhidi yetu) ee Mola wa walimwengu. Ee Allaah tujaalie tuwe watu wa Qur-aan ambao ni watu wako mahsusi (Uwapendao). Ee Allaah ijaalie Qu-raan kuwa rafiki mwandani duniani, na kaburini iwe ni yenye kutuliwaza, iwe nuru katika Asw-Swiraatw, na iwe kiombolezi Siku ya Qiyaamah, na tuambatane nayo Peponi, na iwe sitara na kizuizi cha Moto. Na iwe dalili katika kila kheri na kiongozi kwa Ukarimu Wako ee Mbora wa wanaokirimu. Rahmah na amani zimfikie Mtume wetu Muhammad na Maswahaba zake kwa amani za wingi. 31 www.alhidaaya.com Éb>u‘ ¬! ߉ôϑptø:$#uρ ∩⊇∇⊇∪ šÎ=y™ößϑø9$# ’n?tã íΝ≈n=y™uρ ∩⊇∇⊃∪ šχθàÅÁtƒ $¬Ηxå Í﨓Ïèø9$# Éb>u‘ y7În/‘u z≈ysö6ß™ ∩⊇∇⊄∪ šÏϑn=≈yèø9$# 32 www.alhidaaya.com
Podobné dokumenty
24. Nguvu za Uponyaji za Ushirika Mtakatifu
yamekamilika, na kwamba hakuna haja zaidi ya kuudumisha uponyaji. Ni hatari sana kufikiri kwamba “utunzaji wa baadaye” hauhitajiki. Kumbuka, Yesu alionya: “Angalia umekuwa mzima, usitende dhambi te...
Více